Fasihi Simulizi; Nyambi
Karibu tena katika mwendelezo wetu wa makala zinazohusu fasihi ya kiswahili Sanifu. Katika makala yetu ya leo tutajadili kuhusu nyambi. Ambapo tutaona maana yake pamoja na tanzu zake.
Nyambi ni nini?
Kwanza kabisa tanapaswa kutambua kuwa neno nyambi ni wingi ambapo umoja wake ni WAMBI. Sasa wambi ni nini?
Wambi ni mzungumzo yaliyo na usanaa ndani yake. Huzingatia muktadha, muundo na mtiririko. Humfanya hadhira aendelee kusikiliza kwani huvutia na kuamsha msisimko fulani. Kama vile vicheko, hasira, shangwe n.k
TANZU ZA WAMBI
HotubaMalumbano ya wataniMizaha Maombi
HOTUBA
Hotuba ni mazungumzo rasmi yanayotolewa na mgeni rasmi kwa hadhira. Mazungumzo hayo hujawa vitendawili, misemo, simo na mbinu nyingi za kisanaa. Hotuba hutolewa sehemu rasmi na kwenye matukio rasmi kama...