Karibu tena katika makala zetu zinazoegemea nukuu za kidato cha nne. Leo tutajadili kuhusu lahaja za Kiswahili Sanifu.
Lahaja ni nini?
Lahaja ni uzungumzaji tofauti wa lugha moja. Lahaja za lugha moja hutofautiana kimatamshi, kimiundo na kimsamiati. Hizi hutokea katika lugha yoyote yenye wazungumzaji wengi. Kiswahili ni moja kati ya lugha ambazo zina wazungumzaji wengi. Kutokana na hili lugha hii ina lahaja nyingi. Mfano wa lahaja za Kiswahili ni Kimtang’ata, Kingazija, Kimvita, Kigwana n.k.
AINA ZA LAHAJA
Lahaja zinaweza kugawanywa katika aina tatu ambazo ni:
- Lahaja za Kijiografia / Kitarafa
Hizi ni lahaja ambazo hujinasibisha na mahali. Kutokana na lahaja hizi tunatambua mahali mtu atokako. Kwa mfano; Lahaja ya Kiunguja hupatikana Unguja, Kimgao – Kilwa, Kiamu – Lamu n.k.
- Lahaja za Kijamii
Hizi ni lahaja zinazotambulisha kundi la mtu katika jamii. Kutokana na hili tunaweza kumtambua mtu kama anatoka katika tabaka la juu au la chini, ana weredi gani (kama ni; mwalimu, daktari, mwanasheria n.k), mtu wa mjini au wa kijijini n.k.
- Lahaja za mtindopeke/Lahaja za Nafsi
Hizi ni lahaja ambazo hutofautisha baina ya mtu mmoja na mwingine. Kwa kutumia lahaja hizi tunaweza kutambua sauti ya anayezungumza kama ni ya John au Samwel bila hata kuwatazama.
MAMBO YANAYOSABABISHA UTOKEAJI WA LAHAJA
Lahaja huweza kuchochewa na mambo mbalimbali kama yafuatayo;
- Mwachano wa kijiografia
Mambo yanayoweza kusababisha mwachano wa kijiografia ni kama vile; milima mikubwa, misitu, mito, bahari n.k. Mwachano wa kijiografia huweza kupelekea jamii za lugha moja kutokuwa na muwasala. Hivyo basi, jamii zinazozungumza lugha moja zinapoachana kijiografia na kutokuwa na muwasala wa muda mrefu huweza kuibua lahaja za lugha hiyo. Hii inatokana na mabadiliko ya lugha yanayopatikana kwa kila jamii. Mabadiliko haya hutofautiana baina ya jamii hizo, kwani zinakuwa hazina mawasiliano.
- Mwachano wa kijamii
Endapo jamii zinazozungumza lugha moja zikatengana kwa sababu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe, hadhi na imani, lahaja zinaweza kuzaliwa. Jambo hili linaweza kutokea kwa sababu jamii hizo zitakuwa hazina muwasala mzuri, hivyo mabadiliko ya lugha yanayotokea katika jamii moja si lazima yawe sawia na ya jamii nyingine. Utofauti huo huzaa lahaja.
- Mwingiliano wa kijamii
Lahaja huweza kutokea kwa sababu ya mwingiliano wa kijamii. Jamii zinazozungumza lugha moja zinapokuwa na mwingiliano na jamii za lugha nyingine hupokea athari za lugha hiyo. Athari hizo zinasababisha jamii moja kuwa na msamiati mpya ambao haupatikani katika jamii ya lugha sawa.
- Utabaka
Utabaka katika jamii huweza kuzaa lahaja. Katika jamii tunaweza kupata lahaja za tabaka la juu na lahaja za tabaka la chini, lahaja za mjini na lahaja za kijijini, lahaja za kada mbalimbali n.k.
UMUHIMU WA LAHAJA KATIKA LUGHA
- Ni chombo cha mawasiliano
Kwa kuwa lahaja ni lugha iliyokamilika, hutumika katika kupashana habari miongoni mwa wanajamii.
- Hutambulisha jamii
Kwa kutumia lahaja tunaweza kuibaini jamii. Hivyo, kama mwanajamii anazungumza Kingozi tutajua kuwa anatoka eneo la Pate, Kama anatumia Kimtang’ata tutajua anatokea eneo la Pangani n.k.
- Hukuza lugha Sanifu
Msamiati mpya wa lugha Sanifu hutolewa katika lahaja. Hivyo basi, mchango wa lahaja ni kuongeza msamiati mpya katika lugha Sanifu.
- Hupamba lugha
Kwa kuwa wazungumzaji wa lahaja moja hutofautiana na wazungumzaji wa lahaja nyingine, mrindimo wa sauti hutofautiana. Jambo hili huwafanya wageni wafurahie namna watu wa lahaja fulani wanavyozungumza. Katika Kiswahili watu wa Mombasa, Tanga na Zanzibar hufurahisha kuwasikiliza namna wanavyozungumza Kiswahili.
- Huhifadhi historia ya jamii
Lahaja zimebeba tunu ya lugha. Hivyo kwa wanaisimu ili kujua historia ya lugha fulani basi hurejelea lahaja za lugha hiyo. Jambo hili hufanyika kwani lahaja nyingi zinakuwa bado zina uasili wake. Kutokana na hilo, huweza kuelezea kiini cha lugha kwa urahisi.
Mifano ya Lahaja za Kiswahili
LAHAJA | ENEO INAPOZUNGUMZWA | MFANO WA MSAMIATI |
Kingozi | Pate | Ima (simama), Pulika (sikia), Masi (maovu) |
Kiunguja | Unguja Mjini | |
Kihadimu/Kimakunduchi | Unguja | |
Kitumbatu | Unguja Kaskazini | |
Kimrima | Tanga/Pangani/Dar es Salaam/Rufiji/Vanga/Mafia | |
Kimgao | Kilwa | Chichwa (Kichwa), Chikaanguka ( Kikaanguka) |
Kipemba | Pemba | Ganja (siri), zinga (tafuta), tongoa (sema) |
Kimtang’ata | Tanga/Pangani | Oka (choma), jekejeke (wasiwasi), munyu (chumvi), pweta (tafuta) |
Kivumba | Vanga (Kenya) | Vara (pata), vira (pita), avwera (anataka) |
Kimvita | Mombasa | Biti (bichi), Chanda(kidole), vyaa (zaa) Kitwa (kichwa), jimbi (jogoo), kwea (panda) |
Kiamu | Lamu | Iwe (jiwe), mayani (majani), nana (bibi), simbo (fimbo) |
Kipate | Pate | Fadhaa (haraka), kondo (vita), pija (piga), utuku (soko) |
LAHAJA | ENEO INAPOZUNGUMZWA | MFANO WA MSAMIATI |
Chimiini/Chimabalazi | Somalia/Mogadishu | Chala (Kidole), Shikilo (sikio), oloka (nenda) |
Kingazija | Komoro | Mashobo (mikogo), byindua (pindua) |
Kingwana | Zaire | Moya (moja), mayi (maji), nduku (ndugu), njila (njia).. |
Hello excellent website! Does running a blog similar to this
take a large amount of work? I’ve very little expertise in computer programming but I was
hoping to start my own blog soon. Anyways, if you have any ideas or tips for new blog owners please share.
I know this is off topic however I just had to ask.
Thanks!
Your content is excellent%
Inspiring quest there. What occurred after? Take care!
my web bloog … scr888 under maintenance
We are a group of volunteers and opening a new scheme in our community.
Your web site offered us with valuable information to work on.
You haave done a formidable jjob and our entire community will be thankful to you.
Here is myy homepage … 918kiss demo account
For most up-to-date information you have to visit world-wide-web
and on the web I found this website as a best website for newest updates.
I’m gone to say to my little brother, that he should also visit this web
site on regular basis to get updated from latest information. asmr 0mniartist
If you are going for finest contents like I do, only go to see this web site all the time as it provides feature
contents, thanks 0mniartist asmr
Everything is very open with a really clear description of the issues.
It was definitely informative. Your website is extremely helpful.
Thanks for sharing! asmr 0mniartist
Link exchange is nothing else except it is just placing the other person’s web site link on your page
at appropriate place and other person will
also do similar in support of you. asmr 0mniartist